MANJI: MECHI YA JANA ILIKUWA BONANZA, YANGA TUMEPATA FAIDA SIMBA FURAHA TU

Mwenyekiti wa Yanga Bw.Yusuf Manji akiongea na waandishi wa habari
makao makuu ya klabu, kushoto ni makamu mwenyekiti Clement Sanga
Mwenyekiti
wa klabu ya Young Africans Bw. Yusuf Manji amewaomba wanachama, wapenzi
na washabiki wasivunjike moyo kwa matokeo ya jana ya mchezo wa kirafiki
dhidi ya ya Simba SC, mechi iliyochezwa katika dimba la Uwanja wa Taifa
jijini Dar es salaam.
Akiongea
na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga makutano ya mitaa
wa Twiga/Jangwani Manji amesema anajua wanachama, na wapenzi wameumia
sana hakuna aliyefurahishwa na matokeo ya kufungwa mabao 3-1 lakini
isiwakatishe tamaa uongozi unafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza.
"Mechi
ya jana ilikuwa ni bonanza, ndio maana hapakuwa na timu iliyopata
pointi katika mchezo huo zaidi ya kusherehekea, sisi tumepata zawadi ya
milion 98 wakati wenzetu Simba SC wamepata milion 1, hivyo zaidi sisi
tumeendelea kuimarika kiuchumi zaidi wenzetu wameishia kusherehekea"
alisema Manji.
Aidha
amesema wachezaji zaidi ya tisa wa Yanga hawajapata muda wa kupumzika
tangu mwezi Novemba baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi
Kuu kwani walijiungana timu za Taifa na wamekua huko kwa takribani mwezi
mzima bila kupumzika tofauti na wenzetu Simba SC ambao hawana wachezaji
wengi timu ya Taifa.
Manji
pia alisema anawapa hongera timu ya Simba SC kwa kushinda bonanza la
jana, amesema mchezo wa jana walicheza vizuri hivyo wanastahili pongezi
kwa hilo.
Akijibu
maswali ya waandishi wa habari juu ya mapungufu yaliyojitokez katika
mchezo wa jana, amesema kamati husika inayafanyia kazi na kwa kuwa yeye
anasafiri leo kwenda nje ya nchi majukumu yote amemkabidhi makamu
mwenyekiti Clement Sanga mpaka yeye atakaporejea.
Saturday, December 21, 2013
SIMBA NDIYE MTANI JEMBE,YAIONESHA SOKA YANGA, YAICHAPA 3-1
Wachezaji wa Simba na Yanga wakisalimiana.
Kikosi cha Simba.
Kikosi cha Yanga.
Benchi la ufundi la timu ya Simba.
Benchi la Ufundi la Yanga.
Henry Joseph wa Simba (kushoto) akichuana na beki wa Yanga, David Luhende.
Henry Joseph wa Simba (kushoto) akichuana na beki wa Yanga, David Luhende.
Mashabiki wa Simba wakishangilia bao la kwanza la timu yao.
Raha ya ushindi.
Furaha kwa Simba.
Hamisi Kiiza akitafuta mbinu za kumtoka, Ramadhani singano.
Ivo Mapunda akiruka juu kuokoa moja ya hatari langoni mwake.
Mashabiki wa Yanga wakiwa hawaamini kilichotokea uwanjani baada ya kuchapwa 3-1 na watani zao wa jadi Simba.
Juma Kaseja akibembelezwa na Mbuyu Twite baada ya kusababisha
Mmoja wa mashabiki wa Yanga akitolewa nje baada ya kuzimia uwanjani.
Emmanuel Okwi akimtoka beki wa Simba.
Wachezaji wa akiba wa Simba wakishangilia baada ya filimbi ya mwisho.
Kocha wa Simba, Zdravko Logarusic akishangilia baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa 3-1.
Wachezaji wa Simba
wakimnyanyua juu kocha wao, Zdravko Logarusic mara baada ya kumalizika kwa
mchezo maalumu wa Nani Mtani Jembe uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini
Dar es Salaam. Simba ilishinda 3-1.Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe akimkabidhi kombe nahodha wa Simba Haruna Shamte.
MTANI JEMBE: SIMBA VS YANGA - OKWI AANZIA BENCHI - KASEJA AANZA KIKOSI CHA KWANZA
1.Juma Kaseja - 29
2.Mbuyu Twite - 6
3.David Luhende - 3
4.Nadir Haroub "Cannavaro" - 23(C)
5.Kelvin Yondani "Cotton" - 5
6. Athuman Idd " Chuji" - 24
7.Mrisho Ngassa - 17
8.Frank Domayo - 18
9.Didier Kavumbagu - 7
10.Hamis Kiiza - 20
11.Haruna Niyonzima - 8
2.Mbuyu Twite - 6
3.David Luhende - 3
4.Nadir Haroub "Cannavaro" - 23(C)
5.Kelvin Yondani "Cotton" - 5
6. Athuman Idd " Chuji" - 24
7.Mrisho Ngassa - 17
8.Frank Domayo - 18
9.Didier Kavumbagu - 7
10.Hamis Kiiza - 20
11.Haruna Niyonzima - 8
Subs:
1.Deogratius Munishi "Dida" -30
2.Juma Abdul - 12
3.Oscar Joshua - 4
4.Rajab Zahir - 14
5.Reliants Lusajo - 9
6.Nizar Khalfani - 16
7.Saimon Msuva
8. Hassan Dilunga - 26
9.Jerson Tegete - 10
10.Emmanuel Okwi - 25
11. Said Bahanuzi - 11
12.Hamis Thabit - 22
1.Deogratius Munishi "Dida" -30
2.Juma Abdul - 12
3.Oscar Joshua - 4
4.Rajab Zahir - 14
5.Reliants Lusajo - 9
6.Nizar Khalfani - 16
7.Saimon Msuva
8. Hassan Dilunga - 26
9.Jerson Tegete - 10
10.Emmanuel Okwi - 25
11. Said Bahanuzi - 11
12.Hamis Thabit - 22
Sunday, December 21 2013
SIKINDE YAJICHIMBIA BAGAMOYO KUKABILI MSONDO KRISMASI
Na Mwandishi Wetu
HOMA ya pambano la watani wa jadi katika muziki wa dansi nchini kati ya Mlimani Park 'Wana Sikinde' na Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki' litakalofanyika siku ya Krismasi imeanza kupanda kwa bendi hizo kujificha kambini na huku wakipigana vijembe.
Bendi hizo kongwe nchini zinatarajiwa kuonyeshana kazi katika onyesho litakalofanyika kwenye viwanja wa TCC Club Chang'ombe, Temeke Dar es Salaam katika kunogesha sikukuu hiyo ya Krismasi.
Katika kuonyesha wamelipania pambano hilo bendi ya Sikinde tayari imeiendea Msondo wilayani Bagamoyo kwa ajili ya kuweka kambi yao na wamewatahadharisha 'mahasimu' wao hao wasije wakatoa visingizio baada ya kugaragazwa kwenye onyesho hilo.
"Sisi tumeamua kuweka kambi yetu mjini Bagamoyo ambako tutatua viwanja vya TCC kutokea huko ili kuisambaratisha Msondo, na tunataka wajipange sawasawa ili wasije wakatoa visingizio tena kwa maana kama vyombo vipya bendi zote imepewa na Konyagi," Katibu wa Sikinde, Hamis Milambo alisema.
Milambo alisema mashabiki wa dansi wajitokeze kwa wingi kushuhudia namna gani wanavyowachachafya wapinzani wao hao, ikizingatiwa hawajakutana kwa muda tangu mwaka jana.
Upande wa Msondo kupitia Meneja wao, Said Kibiriti, alisema hawana haja ya kutaja mahali kambi yao ilipo isipokuwa wamejiandaa kuwatoa nishai wapinzani wao siku ya onyesho hilo litakaloanza saa nane mchana.
"Sisi hatuna mchecheto wowote na mpambano huo, tunaendelea kujifua kimya kimya mahali ambapo siwezi kupataja kwa sasa," alisema Kibiriti.
Naye muimbaji anayekuja juu wa bendi hiyo ya Msondo alitokea Sikinde, Athuman Kambi, alisema amejipanga kuonyesha umahiri wake katika mpambano huo baada ya kufanya hivyo wakati akiwa Sikinde dhidi ya Msondo kwenye ukumbi wa Diamond na kuwawehusha mashabiki wa muziki wa dansi nchini.
"Najua watu watataka kuona nafanya kitu gani dhidi ya bendi yangu ya zamani iliyonitangaza vyema, wasiwe na hofu waje Desemba 25 waone nini nitakachofanya TCC Club Chang'ombe," alisema Kambi.
Mpambano huo wa Sikinde na Msondo umeandaliwa na kampuni ya Bob Entertainment na Keen Arts chini ya udhamini wa Konyagi, gazeti la NIPASHE, Integrated Communications, CXC Africa na Salute5.
HOMA ya pambano la watani wa jadi katika muziki wa dansi nchini kati ya Mlimani Park 'Wana Sikinde' na Msondo Ngoma 'Baba ya Muziki' litakalofanyika siku ya Krismasi imeanza kupanda kwa bendi hizo kujificha kambini na huku wakipigana vijembe.
Bendi hizo kongwe nchini zinatarajiwa kuonyeshana kazi katika onyesho litakalofanyika kwenye viwanja wa TCC Club Chang'ombe, Temeke Dar es Salaam katika kunogesha sikukuu hiyo ya Krismasi.
Katika kuonyesha wamelipania pambano hilo bendi ya Sikinde tayari imeiendea Msondo wilayani Bagamoyo kwa ajili ya kuweka kambi yao na wamewatahadharisha 'mahasimu' wao hao wasije wakatoa visingizio baada ya kugaragazwa kwenye onyesho hilo.
"Sisi tumeamua kuweka kambi yetu mjini Bagamoyo ambako tutatua viwanja vya TCC kutokea huko ili kuisambaratisha Msondo, na tunataka wajipange sawasawa ili wasije wakatoa visingizio tena kwa maana kama vyombo vipya bendi zote imepewa na Konyagi," Katibu wa Sikinde, Hamis Milambo alisema.
Milambo alisema mashabiki wa dansi wajitokeze kwa wingi kushuhudia namna gani wanavyowachachafya wapinzani wao hao, ikizingatiwa hawajakutana kwa muda tangu mwaka jana.
Upande wa Msondo kupitia Meneja wao, Said Kibiriti, alisema hawana haja ya kutaja mahali kambi yao ilipo isipokuwa wamejiandaa kuwatoa nishai wapinzani wao siku ya onyesho hilo litakaloanza saa nane mchana.
"Sisi hatuna mchecheto wowote na mpambano huo, tunaendelea kujifua kimya kimya mahali ambapo siwezi kupataja kwa sasa," alisema Kibiriti.
Naye muimbaji anayekuja juu wa bendi hiyo ya Msondo alitokea Sikinde, Athuman Kambi, alisema amejipanga kuonyesha umahiri wake katika mpambano huo baada ya kufanya hivyo wakati akiwa Sikinde dhidi ya Msondo kwenye ukumbi wa Diamond na kuwawehusha mashabiki wa muziki wa dansi nchini.
"Najua watu watataka kuona nafanya kitu gani dhidi ya bendi yangu ya zamani iliyonitangaza vyema, wasiwe na hofu waje Desemba 25 waone nini nitakachofanya TCC Club Chang'ombe," alisema Kambi.
Mpambano huo wa Sikinde na Msondo umeandaliwa na kampuni ya Bob Entertainment na Keen Arts chini ya udhamini wa Konyagi, gazeti la NIPASHE, Integrated Communications, CXC Africa na Salute5.
UCHAMBUZI: YANGA Vs SIMBA
Na baraka mbolembole
Kocha mkuu wa Simba, Zdravko Logarusic tayari ameonesha kufanya
mabadiliko katika upangaji wa kikosi chake, huku yule wa timu ya
Yanga, Ernie Brandts akiongeza suala la stamina kwa kikosi chake.
Logarusic alimpanga kiungo, Henry Joseph katika nafasi ya ulinzi wa
kati wakati wa mchezo wa kirafiki dhidi ya KMKM, wikiendi iliyopita na
mchezaji huyo alionesha kiwango kizuri.
Kwa upande wa Yanga, kuwasili nchini na kujiunga na kambi ya timu
hiyo iliyopo katika hotel ya Protea kwa mshambuliaji, Emmanuel Okwi
kunataraji kuongeza ufanisi na makali zaidi safu ya mashambulizi ambayo mara kwa mara kocha, Brandts amekuwa akisema kuwa ni ' butu' na inayopoteza nafasi nyingi za kufunga, Okwi ni silaha ya hatari, huku
ushirikiano wake na washambuliaji Hamis Kizza na Mrisho Ngassa
ukisubiriwa kwa hamu.
MARA YA MWISHO...
April 20, 2003, mabao ya harakaharaka yaliyofungwa na kiungo, Salumu
Athumani, na mshambuliaji, Herry Morris katika dakika za 30 na 32, na
lile la dakika ya pili baada ya kuanza kwa kipindi cha pili la
kiungo-mshambuliaji, Kudra Omary yaliweza kuipatia ushindi wa mabao 3-0 Yanga katika uwanja wa CCM Kirumba, awali wiki mbili nyuma timu hizo zilifungana bao 1-1 katika mchezo wa kwanza wa kirafiki katika uwanja wa Uhuru. Simba ilitangulia kufunga kupitia kwa mshambuliaji Jumanne Shengo Tondola, na Yanga wakasawazisha kupitia kwa kiungo, Mrundi, Mwinyi Rajab.
Kuongezwa kwa Okwi, na Said Dilunga katika kikosi cha Yanga kunaweza
kuwa kumeipa timu hiyo uimara zaidi katikati na bunduki muhimu mbele.
Lakini hakutasahihisha udhaifu mkubwa wa safu ya ulinzi. Kwa kuwa hata mabeki chaguo la kwanza wanapokuwa fiti, safu ya ulinzi huonekana kupwaya, waliruhusu mabao matatu dhidi ya Azam FC, na baadae Simba wakachomoa mabao yao matatu. Nahodha wa kikosi hicho, Nadir Haroub
amekuwa akionesha dhahiri uwezo wake katika mchezo wa ' man to man',
ila si mzuri katika kujipanga na kuzuhia njia za hatari,
David Luhende bado anajaribu kiwango ambacho kilimfanya kuwa mchezaji wakutumainiwa katika nafasi ya ulinzi wa kushoto, Mbuyu Twite ni namba mbilI mzuri, anashambulia na kuzuhia kwa haraka, mtaalamu wa mipira ya kurushwa na mwenye uwezo mkubwa kwa kupiga mipira iliyokufa. Kocha, Brandts mara nyingi alikuwa akipiga kelele kuwa anahitaji mshambuliaji, na golikipa, na tayari amewapata Okwi na Juma Kaseja, ila hakuonekana kudai nyongeza yoyote ya mlinzi, hasa yule wa kati. Ni Kelvin Yondan pekee anayeweza kucheza mfululizo katika kinachoweza kuitwa kiwango cha juu. Uwepo wa washambuliaji kama Betram Mombeki, Hamis Tambwe, Edward Christopher kunaweza kumkumbusha kocha huyo kosa alilolifanya.
SIMBA KAMA BARCELONA, YANGA KAMA REAL MADRID
Barcelona, mara zote huwa wanatoa matokeo ya kushangaza, pale wanapotabiriwa kufanya vyema huwa wanaanguka vibaya, na pele wasipotarajiwa huwa wanafanya maajabu. Wakiwa na mchezaji bora zaidi duniani, mahasimu wao wanao wachezaji wa bei mbaya ndani ya uwanja. Katika mchezo wao wa kwanza wa ' clasico', Real Madrid ilitota mbele ya Barca. Na sasa, pengine uwepo wa Haruna Niyonzima, Okwi, Hamis Kiza, Didier Kavumbagu, Twite, Kelvin, Nadir, Yanga wakawa na thamani kubwa zaidi ndani ya uwanja, kipesa. Ila Simba imekuwa timu yenye vipaji vinavyoendana na utamadunia wao wa mchezo wa pasi za chini chini.
Herry Joseph atasogea katika nafasi ya kiungo wa ulinzi ili kumpisha mlinzi, Donald Musoti kucheza na Joseph Owino. Uchezaji wa Amri Kiemba unaweza kuwa silaha, au maangamizi kwa Simba endapo atakuwa katika kiwango cha juu Simba itaendelea kuwa timu ile ile inayojiamini ikicheza na Yanga, na endapo itatokea kucheza kwa kiwango cha chini, timu itapotea uwanjani kama ilivyokuwa mwezi oktoba, wakati ule Jonas Mkude aliposhindwa kujiamini.
4-3-3
Timu ya Yanga inaweza kuwapanga kwa pamoja, Okwi, Kiza, na Ngassa katika safu ya mashambilizi jambo ambalo litawachanga walinzi wa pembeni wa Simba, ambao kwa sasa hawapo katika viwango vya juu. Simba inataraji kutumia mfumo huo pia, na uwepo wa kiungo Awadg Juma utaunganisha nguvu na viungo, Mkude na Henry, na kuwaacha Tambwe, Mombeki, na Kiemba katika safu ya mbele.
Kwa kuwa ni mechi ambayo Yanga wanaitumia kuipanga timu yao katika usawa, ni wakati mzuri wa kuwapanga pamoja, Chuji, Domayo na Niyonzima katika kiungo ili kuuchezesha mfumo huo kwa mwendo unaotakiwa, kasi na pasi za uhakika, fupi fupi au zile zenye urefu na macho ya kuangaza. Yanga wanao wachezaji hao na Simba kwa sasa ni timu inayotakiwa kujiendesha kwa mfumo wa 4-4-2 kwa kuwatumia mawinga kupiga krosi kwa washambuliaji wao ambao wanaonekana ni wazuri kwa mipira hiyo.
YANGA, JUMA KASEJA GOLINI
Ni kipa mzuri, kama ambavyo ameweza kudhihirisha hilo kwa kipindi cha miaka 11 sasa, Kaseja atasimama katika mchezo wake wa kwanza wa uhakika tangu mwezi, septemba alipoiwakilisha timu ya taifa katika mchezo wa kufuzu kwa fainali za kombe la dunia dhidi ya Gambia. Aliruhusu mabao mawili wakati Yanga iliposhinda kwa mabao 3-2 dhidi ya KMKM ya Zanzibar, wiki iliyopita. Ataongeza kitu katika lango la Yanga na safu nzima ya ulinzi. Kuwakumbusha majukumu yao mara kwa mara walinzi, kucheza mipira ya kona na krosi ambayo iliwapa sare ya 3-3 katika mchezo wa mwisho wa mahasimu hao.